Msheshe Rashid

Msheshe Rashid

Share

Ukurasa wa msese wa kondeni Ukurasa huu waakisi kazi za uandishi unaokuza Kiswahili

23/10/2024

sisi si maua wala,hatukai mabunduki,
sisi si manyau wala,hatupendelei dhiki,
sisi si mabomu wala,zana za kuzima haki,
tupo zaidi ya kito,utu huvai jeuri.

28/03/2024

Kuwa na SUBIRA utahitaji IMANI.
Kuwa na imani utahitaji USULI WA MAMBO
Kuwa nao usuli wa mambo ndio MWANZO WA KUJITAMBUA.
Ishi maisha.

30/03/2022

K**A SITUNGI SHAIRI!!
Ni barua mwafulani,kwako wewe mahiri,
Utungae kila fani,mjuvi na mjasiri,
Leo waja na ughani,wanena bila kipuri,
K**a situngi shairi,nitungayo ni upupu!
/
Awali ninakiri,usemayo ni nasaha,
Ulo mwema na mzuri,tena usionihaha,
Kando na kushika hari,wanikosea furaha,
K**a situngi shairi,nitungayo ni upupu!
/
Sina haja na kaida,k**a ndugu ywapinda,
Yule kaka yule dada,nitungapo namwinda,
Mawi aasi kudoda,k**a mkosa mkanda,
K**a situngi shairi,nitungayo ni upupu!
/
Ni hofu kwa awashwaye,asomapo ywabipu,
Vibaya tumdhaniye,yu jitu bila ya zipu,
Yu mzaha aonaye,eti nafuma majipu,
K**a situngi shairi,nitungayo ni upupu!
/
Asijifanye dubu,wa jangwa mgeni,
Asutwapo yu bubu,akitenga masitoni,
Hoja zinapodhurubu,hujitia hamsini,
K**a situngi shairi,nitungayo ni upupu!
/
K**a nakubetua,vina chenga vyakupiga,
Ndipo wajibibitua,kwa kebehi za kukoga,
Mwenzio ninabenjua,hadi tungo zajibwaga,
K**a situngi shairi,nitungayo ni upupu!
/
Nakuasia mwenzangu,mimi si k**a wao,
washairi wenye majungu,watungao bila mwao,
Usitunge mapurungu,ukidhani una bao,
K**a situngi shairi,nitungayo ni upupu!

/

Waraka ninaufunga,ninaweka wasalamu,

Iwapo nimedhulumu,mniridhie kaumu,

Mja hapiki sumu,kunywa kisha kulaumu,

K**a situngi shairi,nitungayo ni upupu!

©msese wa kondeni.

16/08/2021

AUGUAYE HUANGALIWA.
//
Tatizo hutatuliwa,tata likatatuka,
Riziki hujuhudiwa,mlo ukatarazika,
Na baya huambuliwa,mbali likajizika,
Dama ndivyo hivyo huwa,muugua hwangaliwa.
//
Ni yakini maridhawa,ganga ganga kuganguka,
Muwele anouguwa,kutunzwa na kutunzika,
Ili nafuu ya kuwa,impate kwa haraka,
Dama ndivyo hivyo huwa,muugua hwangaliwa.
//
Auguaye suluhuwa,anayo tiba tibika,
Si Dawa tu kubuhuwa,na pia kushufahika,
Mathali gahugahu wa,gehugehu akiruka,
Dama ndivyo hivyo huwa,muugua hwangaliwa.
//
Kuseneka kukipowa,Siha na hutatarika,
Ukajyona Umetowa,zito lotasawarika,
Mwenye shida hutasuwa,maono kusaidika,
Dama ndivyo hivyo huwa, muugua hwangaliwa.
//
Khamsani natongowa,tongoo kutafitika,
Vina vinakoma vya Wa,vinasita pia vya Ka,
Takilifu ikikutuwa,kite si dhema kuwika,
Dama ndivyo hivyo huwa,muugua hwangaliwa.
©msese wa kondeni.

Want your business to be the top-listed Business in Nairobi?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Telephone

Address


Bahati
Nairobi

Opening Hours

Monday 09:00 - 17:00
Thursday 09:00 - 17:00