AFro-feeds
Afro-feeds Tunatoa huduma za mifugo pamoja na kutoa Mafunzo ya ujasiliamali na ushauri wa biashara kilimo mifugo Tanzania
10/07/2025
UGONJWA UKITOKEA, MFUGAJI HUJUA KIWANGO CHAKE CHA MAARIFA
“Wengine huogopa kuku wao wakiugua – wengine huongeza uelewa kila tatizo linapotokea.”
CHUKUA HATUA HII LEO:
1. Tengeneza ratiba ya chanjo ya kuku wako – na uifuate kwa ukamilifu.
2. Weka dawa muhimu za dharura – k**a Antistress, Coccidiostat, Glucose.
3. Uliza, jifunze na andika kila ugonjwa utakaokutana nao – si mara zote utampata mtaalamu haraka.
📌 Ugonjwa hauachi taarifa – bali hutoa somo la dhati kwa mfugaji mwenye malengo.
07/07/2025
15/06/2025
Njia sahihi za kutumia dawa za kuua kupe (acaricides) kwenye mifugo.
Tunalenga kupunguza pengo lililopo kati ya maarifa, mitazamo na vitendo vya wafugaji kuhusu udhibiti wa kupe.
📌 Kumbuka:
🔴 Magonjwa yanayosababishwa na kupe bado yanaongoza kwa kuleta hasara kubwa kwenye mashamba ya ng’ombe nchini.
💡 Kwa hiyo, matumizi sahihi ya dawa ya kuua kupe yanaweza kupunguza hadi 70% ya gharama zinazotumika kudhibiti magonjwa ya kupe k**a East Coast Fever, Anaplasmosis n.k.
🟢 Fuga kibiashara, tenga muda wa kujifunza — Afya ya mifugo ni msingi wa faida yako!
Click here to claim your Sponsored Listing.
Category
Contact the practice
Telephone
Website
Address
Arusha
0000