Mr Meshacking
MUNGU NI MWEMA
(GOD IS GOOD)
19/04/2026
Wananchi wa Kata ya Milola, Wilaya ya Ulanga mkoani Morogoro, kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi wakiongozwa na Mkaguzi Msaidizi wa Polisi (A/INSP) Aloyce Andrew, wamefanikiwa kumuua nyoka aliyekuwa akifugwa na kusababisha taharuki kubwa katika eneo la Mavimba, hususan njia panda ya mnadani.
Hofu iliyotokana na uwepo wa nyoka huyo iliwafanya baadhi ya wakazi kushindwa kuendelea na shughuli zao za kila siku za kiuchumi.
Hatua hiyo ilifuatia taarifa kutoka kwa wananchi waliomjulisha mkaguzi huyo kuhusu uwepo wa mtu anayefuga nyoka kwa madhumuni yasiyojulikana.
Tukio hilo lilizua hofu kubwa miongoni mwa jamii, huku wengine wakihisi usalama wao uko hatarini kutokana na uwezekano wa madhara yanayoweza kusababishwa na mnyama huyo.
Akizungumza baada ya tukio hilo, Mkaguzi Aloyce Andrew aliwataka wananchi kujiepusha na imani potofu zinazoweza kuhatarisha amani na utulivu wa jamii.
Pia alimtaka mhusika kuacha mara moja vitendo hivyo, akisisitiza kuwa imani hizo huchangia kudidimiza maendeleo.
Aidha, aliwahimiza wananchi kuendelea kushirikiana na Jeshi la Polisi kwa kutoa taarifa za uhalifu au viashiria vyake ili hatua stahiki zichukuliwe kwa wakati. Mr Meshacking Meshacking Raphael Mtanda
19/04/2026
Rais wa zamani wa Bulgaria, Rumen Radov ambaye amekuwa akitoa ahadi ya kupambana na ufisadi ameonekana kuungwa mkono na raia wengi katika taifa hilo.
Jenerali huyo wa zamani wa jeshi la anga amekuwa akisisitiza kurejesha uhusiano na Urusi na kupinga kutumwa kwa misaada ya kijeshi kwa Ukraine.
19/04/2026
Mr Meshacking Ila ni kweli kabisa😂😂😂
17/04/2026
SERIKALI YATANGAZA ELIMU YA MSINGI YA LAZIMA KUWA MIAKA 10
Dodoma — Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba ametangaza kuanza kwa utekelezaji wa mfumo mpya wa elimu utakaofanya elimu ya msingi kuwa ya lazima kwa kipindi cha miaka kumi, akisema ni sehemu ya mageuzi makubwa yaliyofanywa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Akihitimisha hotuba yake ya bajeti bungeni, Dkt. Nchemba amesema mageuzi hayo ni ya kihistoria kwani mara ya mwisho mabadiliko makubwa ya mfumo wa elimu yalifanyika mwaka 1967, wakati elimu ya lazima ilipopanuliwa kutoka darasa la nne hadi la saba.
Amesema mabadiliko hayo hayaishii kuongeza muda wa masomo pekee, bali yanaambatana na maboresho ya kina yaliyokuwa yakihitajika kwa muda mrefu, ikiwemo kuboreshwa kwa mitaala na miundombinu ya elimu.
“Mheshimiwa Rais ameonyesha ujasiri mkubwa wa kufanya maamuzi haya bila kujali gharama ili kuhakikisha watoto wa Kitanzania wanapata elimu bora,” amesema Dkt. Nchemba.
Ameeleza kuwa maandalizi ya utekelezaji wa mpango huo yamefanyika kwa kiwango kikubwa, huku hatua zilizobaki zikiendelea kukamilishwa ili kuhakikisha utekelezaji wake unakuwa wa mafanikio.
Katika kuimarisha elimu ya ufundi, amesema serikali imeongeza kwa kiasi kikubwa idadi ya shule kutoka takribani tano zilizokuwepo awali hadi zaidi ya 300, zikiwemo shule za awali na za ufundi, ambapo nyingi zina mwelekeo wa masomo ya kihandisi.
Aidha, amesema ujenzi wa madarasa 79,000 umeondoa changamoto ya mfumo wa “second selection” uliokuwa ukiwanyima baadhi ya wanafunzi fursa ya kuendelea na masomo.
Amesisitiza kuwa upanuzi huo wa miundombinu utahakikisha kila mtoto anapata nafasi ya elimu na kuweka msingi wa kuzalisha wataalamu na viongozi wa baadaye.
“Mageuzi haya yataingia katika historia ya nchi yetu na yatakumbukwa kuwa yamefanyika chini ya uongozi wa Dkt. Samia Suluhu Hassan,” amesema. Mr Meshacking Meshacking Raphael Mtanda
Click here to claim your Sponsored Listing.
Category
Contact the public figure
Telephone
Website
Address
Arusha