Initiative for Human Life Development

Initiative for Human Life  Development

Share

Work as partner to the government in order to meet millennium development goals.

Photos from Initiative for Human Life  Development's post 22/09/2020

Taasisi ya IHLD inajipanga kuandaa Maonesho ya Bidhaa za Vikundi ya Wakina Mama Wajasiriamali Wadogo Tabata Segerea.

Photos 26/05/2018

Ushirikiano wako ni Faraja kwa Watoto wetu

Photos from Initiative for Human Life  Development's post 17/05/2016

MDs' wa IHLD

Photos from Initiative for Human Life  Development's post 27/04/2016

Bajeti

Leo nimeona tuzungumze kuhusu bajeti. Hili jambo limekuwa ni gumu sana miongoni mwetu.
Jambo muhimu ni kujua kiasi unachopata kwa mwezi ukitoa kodi zote, kiasi ambacho unatakiwa ukipangie matumizi.
Kwa kawaida yapo matumizi ya aina kuu mbili, haijalishi unafamilia au unaishi mwenyewe na aina hizo ni Matumizi ya Lazima na Matumizi ya Ziada.

Matumizi ya lazima ni kwa mfano:
• Fungu la 10
• Kodi ya nyumba
• Ada za shule
• Chakula
• Mahitaji ya nyumbani mfano; sabuni, mafuta n.k.
• Nauli / mafuta ya gari
• Bili za umeme, maji, msaidizi, mlinzi n.k
• Mawasiliano
• Matibabu
• Akiba
Mahitaji ya ziada ni k**a
• Nguo na viatu
• Michango na zawadi
• Burudani
Tenga kiasi kinachohitajia kwa kila kipengele kwa mwezi. Hakikisha fedha uliyotenga inatosha na usibadili matumizi ya fedha bila sababu ya msingi.

Fedha inayobaki kwa mwezi weka pembeni k**a akiba au unaweza itumia kwa matumizi ya ziada. Mara zote hakikisha umekamilisha matumizi yote ya lazima kabla ya kutumia kwa matumizi ya ziada. Na matumizi ya ziada yanaweza yakawa ni kila baada ya kipindi fulani mfano miezi mitatu hadi sita ili kuweka akiba zaidi kuliko kutumia fedha.
Hakikisha unaifuata bajeti yako k**a ulivyojipangia ili uweze kuona mafanikio.
Mwanzo itakuwa ngumu kidogo ila kadiri unavyojizoeza baadaye itakuwa rahisi sana.
Epuka kununua kitu bila kukipangia bajeti. Tumia pesa yako kwa busara kwa mafanikio yako na familia yako. Pia jitahidi kuwafundisha watoto jinsi ya kutumia fedha kwa uangalifu na kwa bajeti.
Bajeti haimaanishi ianzie kwa wenye uwezo mkubwa hapana, ianzie chini popote pale ili kujikwamua kutoka chini zaidi kwenda juu zaidi kimafanikio

Want your business to be the top-listed Business in Dar es Salaam?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Telephone

Website

Address


Dar Es Salaam
255