Taifa Choice
Online TV For Breaking News, Politics, Sports and Entertainment News.
©2024 Taifa Choice . All Copyright Reserved
10/08/2024
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na maafisa ugani na wanaushirika Ikulu Chamwino, Jijini Dodoma, tarehe 10 Agosti, 2024.
06/08/2024
KATIBU MKUU KIONGOZI AFURAHISHWA NA MAANDALIZI MAZURI YA MAONESHO YA NANE NANE 2024
Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Dkt.Moses Kusiluka ameipongeza Wizara ya kilimo pamoja na Taasisi zake kwa maandalizi mazuri ya Maonesho ya Kimataifa ya Nane Nane alipotembelea na kujionea Teknolojia mpya za uzalishaji pamoja na Tafiti mbali mbali za Kilimo.
Balozi Dkt. Kusiluka amayasema hayo leo tarehe 6 Agosti, 2024 alipotembelea katika Maonesho ya Kimataifa ya Nane Nane katika viwanja vya Nzuguni jijini Dodoma akiambatana na Katbu Mkuu Wizara ya Kilimo, Bw. Gerald Mweli na Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Prof. Riziki Shemdoe.
Aidha Katibu Mkuu Kiongozi amewaalika wananchi kuja katika Maonesho hayo kujifunza Teknolojia mbali mbali za kilimo pamoja na mnyororo mzima wa thamani.
Kwa upande mwingine Balozi Dkt. Kasiluka amesema kuwa hivi sasa kilimo ni biashara kubwa na teknolojia zinazotumika ni za kisasa ambapo ametoa wito kwa vijana kujihusisha na usindikaji wa kisasa wa bidhaa za kilimo kwani kilimo kina fursa lukuki.
MAONESHO YA NANE NANE 2024 NI TOFAUTI NA NANE NANE ZILIZOTANGULIA
Wananchi mbalimbali waliohudhuria Maonesho ya Nane Nane 2024 katika Viwanja vya Nzuguni jijini Dodoma wamepongeza maandalizi mazuri ya Maonesho hayo ya Kimataifa ya Kilimo, Uvuvi na Ufugaji yaliyofunguliwa na Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa jana Agosti 01, 2024 huku yakitarajiwa kufungwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Agosti 08, 2024 (88)
"Nimefika hapa kwenye maonesho ya Nane Nane 2024, nimekuta mabadiliko makubwa sana, tuna kila sababu ya kumpongeza Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, Makamu wa Rais, Waziri Mkuu, Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Kilimo kwa jitihada zao katika kuwezesha maonesho ya Nane Nane 2024 kuwa hivi, kumejengwa tofauti sana" - Alisema Merkiori Tesha, baada ya kutembeela mabanda mbalimbali viwanja vya 88 Nzuguni Dodoma.
Kwa upande wake, Zaina Mwakijazi, Mkazi wa Makulu Dodoma, yeye amesema Nane Nane ya Mwaka huu imekuwa na maandalizi makubwa zaidi tofauti na miaka iliyopita kwanzia kwenye mazingira lakini pia wafanyabiashara wamejitokeza kwa wingi sana na kuna vitu vingi vizuri.
Click here to claim your Sponsored Listing.
Category
Address
Dodoma