Newjerusalem.chc

Newjerusalem.chc

Share

𝐖𝐡𝐚𝐭𝐬𝐀𝐩𝐩 ☏︎ +255 692107628

25/04/2026

VILIO VYA TAWALA MAMA Upendo Nkone Akimshukuru Mungu

22/04/2026

KILA MAUMIVU UNAYOPITIA NI YA MUDA MFUPI TU – MUNGU ATAKUSAIDIA

Bwana Yesu Kristo Asifiwe, Mwana wa Mungu aliye hai.

Inawezekana leo moyo wako umejaa huzuni na maumivu. Inawezekana umechoka kwa sababu ya mambo unayopitia. Labda umeomba sana lakini bado hali haijabadilika. Labda umefika mahali unasema moyoni, “Je Mungu kweli ananiona?”

Leo nataka nikutie moyo kwa Neno la Mungu:
Maumivu unayopitia si ya milele — ni ya muda mfupi tu. Mungu atakuinua.

Biblia inasema:
“Maana mateso yetu mepesi yaliyo ya muda mfupi yatutengenezea uzito wa utukufu wa milele uzidio kuwa mwingi sana.”
(2 Wakorintho 4:17)

Hii ina maana kwamba maumivu yako hayataishi milele. Kuna siku yataisha na Mungu atageuza hali yako.

1. MAUMIVU YA MAHUSIANO

Kuna watu wanaumia sana kwenye mahusiano.
Labda uliwapenda watu kwa moyo wako wote lakini walikuumiza. Labda uliamini mtu lakini akakusaliti.

Maumivu ya mahusiano yanaweza kumfanya mtu akate tamaa kabisa.
Lakini Biblia inasema:

“Bwana yu karibu na waliovunjika moyo, huwaokoa waliopondeka roho.”
(Zaburi 34:18)

K**a moyo wako umevunjika leo, ujue Mungu yupo karibu sana na wewe.
Ana uwezo wa kuponya moyo wako na kukupa mwanzo mpya.

2. MAUMIVU YA KUCHEKWA NA KUDHARAU

Watu wengi wanaumia kwa sababu ya kudharauliwa.

Labda watu wanasema:

“Huyu hawezi kufanikiwa.”
“Huyu hana kitu.”
“Huyu maisha yake yameharibika.”

Lakini kumbuka: watu waliomcheka Yusufu walikuja baadaye kumuinamia.
Biblia inasema:

“Bwana huwainua maskini kutoka mavumbini, na mhitaji humwinua kutoka jalalani.”
(Zaburi 113:7)

Wale wanaokucheka leo wanaweza kushangaa kesho Mungu atakapokuinua.

3. MAUMIVU YA KUONEWA NA KUSINGIZIWA

Kuna maumivu makubwa sana ya kuonewa au kusingiziwa.

Unaweza kuwa hujafanya kosa lolote lakini watu wanakusemea vibaya.
Wengine wanakupaka matope ili kukuharibia jina.
Lakini Mungu anaona na anajua ukweli.

Biblia inasema:
“Silaha yoyote itakayofanyika juu yako haitafanikiwa, na kila ulimi utakaoinuka juu yako katika hukumu utauhukumu kuwa mkosa.”
(Isaya 54:17)

Mungu mwenyewe atasimama kutetea haki yako.

4. MAUMIVU YA KUKATALIWA NA KUBEZWA

unaweza ukawa ni miongoni mwa watu wengi ambao wamekataliwa katika maisha.

Wengine walikataliwa na ndugu zao.
Wengine walikataliwa kwenye kazi.
Wengine walikataliwa kwenye mahusiano.
Lakini hata Yesu Kristo alikataliwa.

Biblia inasema:
“Jiwe walilolikataa waashi limekuwa jiwe kuu la pembeni.”
(Zaburi 118:22)

Hata k**a watu wamekukataa, Mungu anaweza kukufanya uwe wa thamani kubwa sana.

5. MAUMIVU YA UMASIKINI

Umasikini unaweza kumfanya mtu ajisikie hana thamani.
Lakini ujue Mungu hubadilisha hali za watu.

Biblia inasema:
“Baraka ya Bwana hutajirisha, wala haiongezi huzuni pamoja nayo.”
(Methali 10:22)

Mungu anaweza kubadilisha maisha yako ghafla.

6. MAUMIVU YA MAGONJWA

Kuna watu wanaumizwa na magonjwa ya muda mrefu.
Wengine wamezunguka hospitali nyingi bila kupata majibu.

Lakini Biblia inasema:
“Yeye ndiye ayaponyae magonjwa yako yote.”
(Zaburi 103:3)

Hakuna ugonjwa uliomshinda Mungu.

7. HATA HILI LITAPITA

Kila hali ya maisha huwa na mwisho.
Biblia inasema:

“Kilio chaweza kukaa usiku kucha, lakini asubuhi furaha huja.”
(Zaburi 30:5)

Usiku unaweza kuwa mrefu, lakini asubuhi lazima ifike.

HITIMISHO
Kwenye hitimisho Nataka ujue jambo moja muhimu sana:
Hali yako ya sasa si mwisho wa maisha yako.
Mungu anaweza:
~kubadilisha maisha yako
~kukuponya
~kukutetea
~kukufanikisha
~kukurudishia furaha yako

Biblia inasema:
“Nayajua mawazo ninayowawazia ninyi, asema Bwana, mawazo ya amani wala si ya mabaya, kuwapa ninyi tumaini siku zenu za mwisho.”
(Yeremia 29:11)

Kwa hiyo USIKATE TAMAA.
Mungu bado ana mpango mzuri juu ya maisha yako.

MAOMBI
K**a unapitia maumivu yoyote katika maisha yako, nataka kukuombea.

Tuma ombi lako la maombi au maelezo ya changamoto unayopitia kupitia WhatsApp:

+255 692 107 628
Pastor Frank Mgaya

Tutakuombea, na Mungu atakusaidia.
Kumbuka:

Maumivu yako ni ya muda mfupi tu. Mungu atakuinua.
Bwana akubariki sana.

By PASTOR FRANK MGAYA

22/04/2026

WIMBO UNAITWA SAUTI NDANI YA MACHOZI kutoka kwake Rev.

13/04/2026

MWAMINI MUNGU

Want your place of worship to be the top-listed Place Of Worship in Dodoma?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Telephone

Website

Address


Dodoma