Taifa Digital Forum
Tunahusika na Uzalishaji wa Habari na Makala zinazohusu mstakabali wa Serikali ya Tanzania na Wananchi wake | Kufanya Mahojiano na watu mashuhuri.
22/11/2024
NUKUU:
"Waambieni watu wema wao na uzuri wao, inaweza wasaidia na kuwapa nguvu ya kuendelea kutenda mema kuliko kuja kueleza baadae wakiwa hawana uwezo wa kusikia wala kuona" - Samweli Sasali .samsasali360 : Mwanahabari.
WAFUGAJI WAMFAGILIA RAIS SAMIA KWA KUMALIZA MIGOGORO YA ARDHI
Jamii ya wafugaji wa wilaya ya Kilosa imempongeza Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kutatua changamoto ya migogoro ya ardhi ambayo kwa muda imekuwa ikiwatesa wakulima na wafugaji hasa katika wilaya ya Kilosa ambapo mara kwa mara wafugaji na wakulima walikuwa wakishambuliana kufuatia kugombania ardhi.
Akizungumza kwa niaba ya wafugaji wengine wakati ziara ya Rais ilipofika wilaya ya Kilosa mwananchi Shaka Stoni ambaye ni mfugaji amesema,
"Kwa niaba ya kilosa na wafugaji wote niseme sisi wafugaji tunamfurahia mama kwa kuwa tangu alipokaa kwenye kiti hatujawahi kuona ugomvi kabisa na bei ya mifugo imeongezeka sisi k**a wafugaji tunampenda sana na tunataka aendelee kwa sababu mama ndio chaguo letu".
Click here to claim your Sponsored Listing.
Category
Contact the business
Website
Address
Dodoma