Mbeya Zonal Referral Hospital
Ukurasa rasmi wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya
02/06/2026
Shukrani:
Ujio wenu na maneno yenu ya heri yameendelea kutupa chachu na hamasa ya kutoa huduma bora, zenye viwango na upendo kwa jamii yetu.
28/05/2026
MHE. JOSEPHINE MANASE APONGEZA HUDUMA ZA KIBINGWA BILA MALIPO MZRH, MBEYA CITY EXPO 2026.
Mkuu wa Wilaya ya Kyela, Mhe. Josephine Manase leo ametembelea banda la Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya (MZRH) katika Maonesho ya Nne ya Biashara na Kilimo ya Mbeya City Expo 2026 na kuwapongeza wataalamu wa afya kwa kutoa huduma bora za kibingwa na kibobezi kwa wananchi bila malipo yoyote.
Mhe. Manase amesema: "Nawapongeza sana wataalamu wetu wa MZRH kwa moyo wenu wa uzalendo na weledi mkubwa mnaouonesha hapa maoneshoni. Kusogeza huduma hizi za kibingwa na kibobezi bila malipo ni ukombozi mkubwa kwa wananchi wa Kyela na Mkoa mzima wa Mbeya, kwani inawaondolea adha ya kusafiri umbali mrefu na kuwapunguzia gharama."
Click here to claim your Sponsored Listing.
Category
Contact the organization
Website
Address
Hospital Street
Mbeya