Midnight graphics
Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Midnight graphics, Digital creator, Mbeya tz, Mbeya.
02/06/2026
Asante sana Wadau wote wa Mazingira ambao Walijitokeza Kutembelea Booth yangu na Kujifunza Namna Gani Tunaweza Kuthibiti Taka Katika Jamii yetu ya Tanzania kupitia Njia ya Kisasa Na Rahisi.
02/06/2026
Nilipata Nafasi ya Kuhudhuria Maonesho ya Siku ya Mazingira Duniani sambamba na Miaka 40 ya NEMC ,
Ambapo Nilifika K**a Exhibitor wa Mfumo wa Kisasa wa Kidijitali utakao Saidia Kuondoa Adha ya Taka za Kielektroniki katika Mazingira Na Kuweka Nchi yetu Salama .
Ni furaha Kubwa Kusindikizwa na Mbunge wa Vyuo na Vyuo Vikuu zanzibar .zeyanahamid Lakini Pia Natambua Heshima na Nafasi Niliyopewa na Mhe waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Maonesho Mhe.Mhandisi Hamadi Yussuf Masauni
Hii Ni Kubwa sana kwangu na Imenijenga Katika Uzalendo Na Kupenda Usafi wa Nchi Yangu
06/05/2026
Leo nimepata nafasi ya kutimiza wajibu wangu k**a Waziri wa Habari, Mawasiliano na Ubunifu SUZASO, kwa kuwasilisha changamoto na maoni ya wanafunzi wa SUZA mbele ya Rais wa Serikali ya Wanafunzi, Ndg. Asia Ramadhan Khamis.
Nikiwa ninawakilisha Skuli ya Kompyuta Sayansi na Teknolojia ya Habari, nimewasilisha hoja zinazogusa moja kwa moja maendeleo ya taaluma yetu—kuanzia miundombinu ya teknolojia, mazingira ya kujifunzia hadi fursa za ubunifu na ujuzi wa kisasa.
Hii si tu hatua ya kuwasilisha changamoto, bali ni kusimamia sauti ya wanafunzi na kuhakikisha mahitaji yao yanapata nafasi stahiki katika ngazi za maamuzi.
Ninaamini kuwa mawasiliano sahihi ni msingi wa mabadiliko—na ubunifu ni nguvu ya kesho.
18/04/2026
Ofisi ya Mbunge Viti Maalum Kundi la Vyuo na Vyuo Vikuu Zanzibar imeandaa kongamano maalum lenye lengo la kuunganisha ubunifu na fursa kwa wanafunzi wa vyuo na vyuo vikuu.
Mimi Hamidu Nchalikwao Waziri wa Habari Mawasiliano na Ubunifu SUZASO, Idara ya Habari Ofisi ya Mbunge viti Maalumu vyuo na Vyuo Vikuu zanzibar
Nitashiriki ☑️
Wanafunzi wote mnakaribishwa kuhudhuria na kushiriki kikamilifu.
📅 24 Aprili 2026
⏰ 03:00 Asubuhi
📍 Dkt. Shein Hall, SUZA Tunguu
Huduma zote ni bure:
🚍 Free Transport
🎟 Free Entry
🍽 Free Lunch & Drinks
mnakaribishwa
kushiriki.
TEYA
13/04/2026
Waziri wa Habari, Mawasiliano na Ubunifu wa SUZASO, Ndg. Hamidu Nchalikwao, ameibuka mshindi wa tuzo ya Rising Star in Science and Technology katika Tanzania Youth Emerging Awards (TEYA).
Hamidu amejizolea sifa kubwa katika tasnia ya ubunifu wa picha (graphics design), ambapo hapo awali aliwahi kushinda tuzo ya Best Graphics Designer Mkoa wa Mbeya, pamoja na Best Graphics Designer SUZASO Awards 2025.
Tuzo hiyo imetolewa kwa kutambua mchango wake katika kukuza ubunifu wa kidijitali, mawasiliano ya kisasa, na uongozi wake ndani ya SUZASO katika sekta ya habari na ubunifu.
03/02/2026
Imekua ni Heshima kubwa na Historia kuandikwa Viongozi kutoka Serikali za Wanafunzi Vyuo MbaliMbali Mbali Tanzania Bara na Visiwani Kuonana ,kwa Ajilibya Tulio Maalumu la Semi Final ya Inter University Talents Competition season 03 .
Kulia ni Waziri wa Habari na Mawasiliano Serikali ya Wanafunzi Chuo kikuu Cha Taifa Zanzibar SUZA Mhe.Hamidu Nchalikwao.(SUZASO).
Anaefuata ni Rais wa Serikali ya Wanafunzi Chuo kikuu Cha Afya Muhimbili Mhe.Nzengwa Mahela (MUHASSO).
Anaefuata ni Makamu wa Rais Serikali ya Wanafunzi Chuo cha Usafirishaji Tanzania NIT Mhe.Halima Mbaruku Masoud .m.masudi (SONIT).
Lakini pia Kulia ni Rais wa Serikali ya Wanafunzi Chuo cha KCMC .
Hakika INTERUNUVERISTY TALENTS COMPETITION ✨
Ni Jambo la kujivunia na la Kihistoria ✍️
@kcmcuniversity
03/02/2026
Hongera sana
BEST PRESENTER OF THE YEAR
Zari Awards 2025
03/02/2026
Hongera sana Kazi nzuri Keep Going on Brother.
Click here to claim your Sponsored Listing.
Category
Address
Mbeya Tz
Mbeya